Vita Vya Ukombozi
Vita vya ukombozi, vilianzishwa
Mji mtakatifu makao ya Bwana
Dhambi ilipoingia kwa ibilisi
Majeshi takatifu walimshinda
Na sisi tutashinda
Kwa damu ya Mwana
Kondoo na kwa neno la,
Ushuhuda wetu
Pale msalabani tuliwezeshwa
Kumshinda shetani, dhambi na mauti
Tena hatutapenda maisha yetu
Tutakubali kuyapoteza vitani
Vita vya ukombozi
Alivishinda
Juu ya msalaba, Yesu Mwokozi
Alitoa tangazo
Yenye ushindi
Hapo aliposema, yote yamekwisha
Vita vya ukombozi
Walivipata
Manabii na mitume, na walimshinda
Mnyama kwa damu ya,
Mwana Kondoo
Na kwa ushuhuda wao mpaka walilala
Vita vya ukombozi
Vya mwana damu
Kati ya Mwana Kondoo
Na mwovu shetani
Vilikuwa vikali
Msalabani
Dunia pia mbingu, vikishuhudia
Njia ya Kalvari
Alikanyanga
Kusudi wewe nami
Tupate wokovu
Mbona wadanganyika,
Unachelewa,
Vita vimetangazwa
Vya mwana adamu
Home