Mwamba Wenye Imara
Mwamba wenye imara
Kwako nitajificha.
Maji hayo na damu
Yaliyotoka humu,
Hunisafi na dhambi,
Hunifanya mshindi.
Kwa kazi zote pia
Sitimizi sheria.
Nijapofanya bidii,
Nikilia na kudhii,
Hayaishi makosa;
Ndiwe wa kuokoa.
Sina cha mkononi,
Naja msalabani;
Nili tupu, nivike;
Ni mnyonge, nishike;
Nili mchafu naja,
Nioshe nisijafa. .
Nikungojapo chini,
Na kwenda kaburini;
Nipaapo mbinguni,
Na kukwona enzini;
Roho yangu na iwe
Rahani mwako wewe.
Home