Enyi Askari Wa Kristo

Enyi askari wa Kristo,
Mlio vitani;
Muwe hodari kwa bidii,
Msishindwe kweli.
Adui zetu washindwe
Na nguvu za Yesu,
Imani ni nguvu zetu,
Hushinda uovu.

Chorus
Imani ni nguvu,
Imani ni nguvu;
Nguvu za utukufu,
Hushinda uovu.

Bendera yake ni pendo,
Upanga ni Neno;
Tuishike njia yetu,
Tufanye vifijo:
Watakatifu wa kale
Wakawa washindi,
Kwa imani ishindayo
Tushinde vitani.

Ashindaye atapewa
Mavazi meupe,
Malaika watamjua
Akitajwa mle;
Tuendelee na pendo
Majeshi tushinde,
Katika Jina la Yesu
Tuishi milele.

Home