Bwana Nieleze
  Bwana nieleze kile kilicho
  kufanya ukaja hapa wakati ule
  Yote ya mbinguni hukuyaona kitu,
  ukaja ishi na viumbe vyako,
 
  Hebu nieleze kwa sauti ya upole,
  akili zangu bwana Ni fupi,
  rudia rudia kama vile kwa mtoto,
  nisisahau hata kidogo
 
  Walipo kusulubisha msalabani
  hakuna aliye kusaidia
  Ukafa kifo cha uchungu na Aibu
  Kwa dhambi iliyokua yangu
 
  Zidi kunionyesha ubaya wa dhambi
  Najua ndio iliyokuua
  Na nigeukapo bwana kutenda dhambi
  Bwana nirudi kwa fimbo yako
 
Home