Aitwa "Wa Simanzi."

Aitwa "Wa Simanzi,"
Mwana wa Mwenye enzi
Mwenye mengi mapenzi!
Nasifiwe Bwana Yesu.

Akawa matesoni
"Mungu Mwana" yakini
Akatoka mbinguni
Nasifiwe Bwana Yesu.

Akapata dhihaka
Mzoea-mashaka
Ndiye yetu sadaka:
Nasifiwe Bwana Yesu.

Tu wenye dhambi sana,
Kwake dhambi hamna:
Na Mungu twapatana:
Nasifiwe Bwana Yesu.

Alikufa Mtini
Akalia dhikini
Sasa yuko mbinguni:
Nasifiwe Bwana Yesu.

Punde atarejea
Yesu kutunyakua
Ndipo tutamwimbia,
Nasifiwe Bwana Yesu."

Home





Next song