Nina Haja Nawe

Nina haja nawe
Kila saa
Hawezi mwingine
Kunifaa.

Yesu nakuhitaji
Vivyo kila saa!
Niwezeshe Mwokozi,
Nakujia.

Nina haja nawe;
Kaa nami,
Na maonjo haya,
Hayaumi.

Nina haja nawe:
Kila hali,
Maisha ni bure,
Uli mbali.

Nina haja nawe,
Nifundishe
Na ahadi zako
Zifikishe.

Nina haja nawe;
Mweza yote,
Ni wako kabisa
Siku zote.

Home





Next song