Ni Mji Mzuri
Ni mji mzuri,
Mbali sana;
Watu wanawiri
Kama jua;
Waimba kwa tamu
Tuna mwema Hakimu:
Sifa na idumu,
Kwake Bwana.
Ni mji mzuri
Twende sote!
Una na fahari
Msikawe!
Raha tutaona,
Dhambi hapana tena:
Hatutaachana
Siku zote.
Ni mji mzuri:
Macho yote
Huko hunawiri
Kama pete;
Baba tutamwona,
Tukifanywa tu wana;
Tumo kupendana
Naye sote.
Ni mji mzuri:
Tusipotee
Na tuwe hodari,
Tuupate!
Tufuze, tutume
Kwa taji na ufalme:
Sifa na zivume
Siku zote.
Home