Nilitembea Gizani
Nilitembea gizani,
Yesu akaona;
Kwa mwanga wa pendo lake,
Giza lilifutwa.
Chorus
Mwanga, mwanga rohoni mwangu,
Mwanga, mwanga kwa njia yangu;
Tangu nimepata wokovu wangu,
Yesu amenijaza kwa mwanga mkuu.
Ninapoenda nuruni,
Mwa upendo wake;
Nashirikiana naye,
Gizani si kwake.
Nikitembea shambani
Ama kwa njiani;
Naona mavuno yake,
Anifanye mvuni.
Atakaporudi tena,
Sitaki kutanga;
Nitamwona Yesu Bwana,
Yeye ndiye Mwanga.
Home