Baba, Mwana, Roho

Baba, Mwana, Roho, Mungu Mwenye enzi,
Kila tukiamka tunakuabudu.
Baba, Mwana, Roho, Mungu wa mapenzi,
Ewe Utatu, tunakusifu.

Baba, Mwana, Roho, wakuaminio
Wanakutolea shukurani zao.
Wakusujudia malaika nao:
Wewe U mwanzo, nawe U mwisho.

Baba, Mwana, Roho, sisi tu gizani,
Utukufu wako haoni mkosa;
U Mtakatifu, nawe U mapenzi,
U peke yako, mwenzio huna.

Baba, Mwana, Roho, Mungu Mwenye enzi,
Ulivyoviumba vyote vyakusifu:
Baba, Mwana, Roho, Mungu wa mapenzi,
Ewe Utatu, tunakusifu.

Home