Sioni Haya kwa Bwana

Sioni haya kwa Bwana
Kwake nitang'ara!
Mti wake sitakana
Ni neno imara!

Chorus
Msalaba ndio asili ya mema,
Nikatua mzigo hapo:
Nina uzima, furaha daima
Njooni kafurahini papo.

Kama Kiti chake vivyo
Ni yake ahadi:
Alivyowekewa navyo
Kamwe havirudi.

Bwana wangu, tena Mungu
Ndilo lake jina!
Hataacha roho yangu
Wala kunikana.

Atakiri langu jina
Mbele za Babaye:
Anipe pahali tena
Mbinguni nikae.

Home





Next song