Una Nafasi kwa Yesu?
Una nafasi kwa Yesu?
Aliyeondoa dhambi;
Abishapo mlango wako,
Umkaribishe ndani.
chorus
Nafasi kwa Mfalme Yesu,
Neno lake ulitii;
Ufungue moyo wako,
Aingie moyoni.
Anasa ina nafasi,
Bali Yesu hawezi;
Kuingia moyo wako,
Mbona wewe humpendi?
Una nafasi kwa Yesu?
Leo akikuita
Usimkatae, mwenzangu,
Ni bora kumwitika.
Home