Nitaonana na Yesu

Nitaonana na Yesu,
Uso kwa uso kweli;
Siku ile shangwe tele,
Nikimwona Mwokozi.

Chorus
Tutaonana na macho,
Huko kwetu Mbinguni;
Na kwa utukufu wake,
Nitamwona milele.

Sasa siwezi kujua
Jinsi alivyo hasa;
Bali atakapokuja,
Nitamwona halisi.

Mbele yake yafukuzwa
Machozi na huzuni:
Kipotovu kitanyoshwa,
Fumbo litafumbuka.

Uso kwa uso! Hakika
Pale pale furaha;
Nitafurahi kabisa,
Nikimwona Mwokozi.

Home