Aliteswa, Aliteswa

Aliteswa, aliteswa,
Msalabani Yesu aliteswa;
Dhambi zangu ameziondoa,
Mahali pangu aliteswa.

Alikufa, alikufa,
Msalabani Yesu alikufa;
Kwa kifo chake nakombolewa,
Kwa kuwa Yesu alinifia.

'Kafufuka, 'Kafufuka,
Kaburini Yesu alitoka;
Nami nimewekwa huru pia,
Kwa kuwa Yesu alifufuka.

Yuko hai, yuko hai,
Mbinguni anaishi Mwombezi;
Daima huniombea mimi,
Kwa kuwa Yesu adumu hai.

Atarudi, atarudi,
Siku moja Yesu atarudi;
Na tumwonapo tutafurahi,
Kwa kupelekwa kwake mbinguni.

Sifa kwake, sifa kwake,
Mbinguni na huimbwa milele;
Kwa furaha, masifu, na shangwe,
Tutamwimbia Yesu milele.

Home





Next song