Nafsi Yangu

Naja mbele zako Bwana,
Mungu wa majeshi,
Najitoa kama dhabihu, iliyo hai,
Nipokee Bwana, ni kiumbe hafifu,
unifanye niwe wako

Unitumie upendavyo,
unitume utakako,
mimi chombo chako Bwana

Nafsi yangu yakutamani,
Bwana kama vile ayala,
atamanivyo maji,
ndivyo nafsi yangu, yakutamani,
nafsi yangu, yakutamani

Niumbie moyo safi, ehe Mungu,
nitilie roho mpya, na dhabiti,
usinipokonye roho wako,
usinitupe mbali nawe,
nirejeshe raha ya wokovu

Sala zangu zisikie,
kilio changu kisikize,
unipe moyo wa kukutii

Nafsi yangu yakutamani,
Bwana kama vile ayala,
Atamanivyo maji,
Ndivyo nafsi yangu, yakutamani,

Ndivyo nafsi, yangu ilivyo
Nafsi yangu, yakutamani

Home