Nafsi Yangu
Naja mbele zako Bwana,
Mungu wa majeshi,
Najitoa kama dhabihu, iliyo hai,
Nipokee Bwana, ni kiumbe hafifu,
unifanye niwe wako
Unitumie upendavyo,
unitume utakako,
mimi chombo chako Bwana
Nafsi yangu yakutamani,
Bwana kama vile ayala,
atamanivyo maji,
ndivyo nafsi yangu, yakutamani,
nafsi yangu, yakutamani
Niumbie moyo safi, ehe Mungu,
nitilie roho mpya, na dhabiti,
usinipokonye roho wako,
usinitupe mbali nawe,
nirejeshe raha ya wokovu
Sala zangu zisikie,
kilio changu kisikize,
unipe moyo wa kukutii
Nafsi yangu yakutamani,
Bwana kama vile ayala,
Atamanivyo maji,
Ndivyo nafsi yangu, yakutamani,
Ndivyo nafsi, yangu ilivyo
Nafsi yangu, yakutamani
Home