Alishuka Kutoka Mbinguni
Alishuka kutoka mbinguni,
Yesu Bwana wangu;
Kwangu akaziondoa dhambi,
Napendwa na Mungu.
chorus
Sina budi kumpenda,
Yesu Mwokozi,
Sina budi kumpenda,
Ndiye Mkombozi.
Sistahili kupata neema,
Neema yake mkuu;
Na badala yangu akateswa,
Kwa uovu wangu.
Yesu yu Mwema kuliko wote,
Hupenda kwa haki;
Nauona utukufu wake,
Na Mungu mbinguni.
Home
Next song