Yesu Nakupenda
Yesu nakupenda, U mali yangu,
Anasa za dhambi sitaki kwangu:
Na Mwokozi aliyeniokoa,
Sasa nakupenda, kuzidi pia.
Moyo umejaa mapenzi tele
Kwa vile ulivyonipenda mbele,
Uhai wako ukanitolea
Sasa nakupenda, kuzidi pia.
Ulipoangikwa Msalabani
Tusamehewe tulio dhambini;
Taji ya miiba uliyoivaa
Sasa nakupenda, kuzidi pia.
Niwapo hai, niwapo maiti,
Kupendana nawe kamwe siachi;
Hari za kifo zikinienea,
Sasa nakupenda, kuzidi pia.
Home