Nimejazwa na Furaka

Nimejazwa na furaha,
Tangu Roho akaja;
Hukaa nasi daima,
Moyoni mwa hakika.

Chorus
Utulivu wa rohoni
Umekaa moyoni;
Roho wa Bwana aniletea
Utulivu moyoni.

Atuleteaye Uzima
Ni Roho Mtakatifu;
Kutoamini aondoa,
Kuchoka ageuza.

Kama mvua inyeshavyo,
Kama jua angani;
Ndivyo tumepewa Roho,
Kutoka mbinguni.

Ni wokovu wa ajabu
Kumwona uso wake;
Makao makamilifu
Tumepewa na Yeye.

Home