Umealikwa

Umealikwa, uje sasa,
Karamu imeandikwa;
Uje sasa uliyechoka,
Na utabarikiwa.

Chorus
Itika mwaliko,
Kwa awaye yote;
Mungu na asifiwe,
Kwa wokovu wake.

Umealikwa, uje sasa,
Uje utakaribishwa;
Na utaheshimiwa sana,
Utaketi na Bwana.

Umealikwa, uje sasa
Uje anakungojea;
Usikawie, uje leo,
Labda utachelewa.

Umealikwa uje sasa,
Acha masumbuko yote;
Uje ule pendo la Mungu
Tapata utulivu.

Home





Next song