Kutakuwa na Baraka

Kutakuwa na baraka,
Hiyo ni Neno lake;
Kutakuwa na faraja,
Bwana hutoa kwake.

Chorus
Baraka nyingi,
Baraka twahitaji;
Tumepokea kiasi,
Bali twataka nyingi.

Kutakuwa na baraka,
Ufufuo twataka;
Kwa mabonde na milima.
Mungu anyeshe mvua.

Kutakuwa na baraka,
Zitumwagie Bwana:
Kuburudishwa twataka,
Na mvua yako Bwana.

Kutakuwa na baraka,
Laiti zianguke;
Haja zetu twaungama,
Yesu, utusikie.

Kutakuwa na baraka,
Tukimjua na kumtii;
Tena tutaburudishwa,
Tukimpa nafasi.

Home





Next song