Mtazame Huyo

Mtazame Huyo!
Aliyeangikwa juu
Hivi sasa upate ishi.
Mwenye-dhambi dhaifu,
mtazame tu
Wala usifanye tashwishi.

Chorus
Tazama! Tazama! uishi!
Mtazame Huyo aliyeangikwa Juu
Hivi sasa upate ishi.

Kama siye Kondoo
Mwondoa-dhambi,
Na makosa yako ya mumu!
Kama deni zetu zote hakulipa
Mbona imemwagika damu?

Si kutubu na sala ikomboayo
Ila damu ndiyo salama;
Na aliyemwaga aweza, sasa,
Dhambi zako kukufutia.

Usiwe na shaka,
Mungu amesema,
Hakuna alilolisaza;
Hapo alipokuja alitimiza,
Kazi zote alizoanza.

Basi twae uzima kwa kufurahi
Upokee kwa Bwana, sasa,
Ujijue hakika kwake kuishi
Yesu, aishiye kabisa.

Home





Next song