Mungu Awe Nanyi Daima

Mungu awe nanyi daima;
Hata twonane ya pili,
Awachunge kwa fadhili,
Mungu awe nanyi daima.

Chorus
Hata twonane huko juu,
Hata twonane kwake kwema;
Hata twonane huko juu,
Mungu awe nanyi daima.

Mungu awe nanyi daima;
Ziwafunike mbawaze,
Awalishe, awakuze;
Mungu awe nanyi dairna.

Mungu awe nanyi daima;
Kila wakati wa zani
Awalinde hifadhini;
Mungu awe nanyi daima.

Mungu awe nanyi daima;
Awabarikie sana,
Awapasulie kina;
Mungu awe nanyi daima.

Home





Next song