Chini ya Mizigo ya Dhambi
Chini ya mizigo ya dhambi,
Watu wengi walemewa;
Bali waweza kufurahi,
Wakipokea uzima.
Chorus
Uzima, uzima,
Yesa ndiye Mtoaji;
Uzima daima,
Asifiwe Mwokozi.
Mwenye mizigo usishike
Huzuni zilizo tele;
Ufungue moyo ujazwe
Na uzima wa milele.
Kama mto ulivyotoka
Mlima, kutuliza bonde;
Ndivyo kutoka Msalaba,
Uko uzima wa tele.
Nehi kavu igarikishwe,
Na tupate ufufuo;
Tusiogope, tutakaswe,
Kutangaza ufufuo.
Home