Deni Yangu ya Dhambi

Deni yangu ya dhambi,
Yesu amelipa;
Kwake Msalabani
Nilipewa uzima.

Chorus
Deni ya dhambi,
Msalabani;
Ilimalizikia
Ni huru kabisa.

Bwana Yesu asema,
"Mwanangu dhaifu,
Uwezo na ushindi,
Hupatikana kwangu."

Bwana, kweli naona,
Nguvu zako pekee;
Huondoa ukoma,
Niwe kipya kiumbe.

Sina wema moyoni,
Nidai neema;
Nakubali kabisa,
Kwa damu kusafiwa.

Hata huko Mbinguni,
Miguuni pake;
"Yesu alinifia,"
Nitaimba milele.

Home





Next song