Ebu Nieleze
Bwana niambie kile kilichokufanya
Ukaja huku wakati ule
Yote ya mbinguni huku yaona kitu
Ukaja ishi na watu wako
Bwana
Ebu nieleze kwa sauti ya upole
Akili zangu Bwana ni fupi
Rudi rudia kama vile kwa mtoto
Nisisahau hata kidogo
Walipokusulubisha msalabani
Hakuna aliyekusaidia
Ukafa kifo cha uchungu na aibu
Kwa dhambi zisizo kuwa zako
Zidi kunionyesha ubaya wa dhambi
Najua ndizo zilizokuuwa
Na ningekuwapo Bwana kutenda dhambi
Ebu nirudishe kwa fimbo yako
Bwana
Ebu nieleze kwa sauti ya upole
Akili zangu Bwana ni fupi
Rudi rudia kama vile kwa mtoto
Nisisahau neno lako
Bwana niambie kwa sauti ya upole
Akili zangu zikuelewe
Rudia rudia kama vile kwa mtoto
Nisisahau hata kidogo
Home