Bwana Ni Mchungaji

Bwana ni mchungaji wangu,
Sitapungukiwa kitu
Hun'laza penye majani mabichi,
Huniongoza kwa maji matulivu

Hunihuisha nafsi yangu,
Hun'ongoza kwa njia za haki
Nipitapo bondeni mwa mauti,
Sitaogopa wewe u nami

Hakika wema nazo fadhili zitanifuata mimi,
Nitakaa nyumbani mwa Bwana,
Siku zote za maisha yangu

Gongo lako na fimbo yako,
Vitanifariji mimi
Waandaa meza mbele yangu,
Machoni pa watesi wangu

Hakika wema nazo fadhili zitanifuata mimi,
Nitakaa nyumbani mwa Bwana,
Siku zote za maisha yangu

Home





Next song