Nimeifikia Nchi

Nimeifikia nchi,
Ya nafaka na asali;
Mwanga hung'ara daima,
Na usiku umekoma.

Chorus
Nchi nzuri, nchi nzuri,
Nasimama mlimani,
Naona nchi ya mbali
Iliyowekwa tayari;
Niitazamie pwani
Ya nchi yangu mbinguni.

Mwokozi wangu yu nami,
Twashirikiana kweli;
Aniongoza mkononi,
Nifike kwake mbinguni.

Nazisikia sauti
Za malaika mbinguni,
Wamwimbie Bwana sifa
Na wale waliookoka.

Home