Yesu Kwetu Ni Rafiki

Yesu kwetu ni Rafiki,
Hwambiwa haja pia;
Tukiomba kwa Babaye
Maombi asikia;
Lakini twajikosesha,
Twajitweka vibaya;
Kwamba tulimwomba Mungu
Dua angesikia.

Una dhiki na maonjo?
Una mashaka pia?
Haifai kufa moyo,
Dua atasikia.
Hakuna Mwingine Mwema
Wa kutuhurumia:
Atujua tu dhaifu;
Maombi asikia

Je, hunayo hata nguvu,
Huwezi kwendelea,
Ujapodharauliwa
Ujaporushwa pia.
Watu wangekudharau,
Wapendao dunia,
Hukwambata mikononi,
Dua atasikia.

Home





Next song