Kichwa Kilivikwa Miiba
Kichwa kilivikwa miiba,
Kina enzi sasa;
Anayo taji ya sifa,
Ilivyompasa.
Pake ni pa juu sana
Jumbe wa majumbe;
Yesu, Bwana wa mabwana,
Nuru za viumbe.
Nyemi za wakaao juu,
Nyemi za wa chini,
Alionya pendo kuu,
Jina la sirini.
Mti wa aibu sana
Kwao una wema;
Wanayo raha daima
Kwa kifo cha Bwana.
Chini wanayo dhiki kuu;
Kwako wana enzi;
Kwao furaha, pato kuu
Ni yake mapenzi.
Mti wa kufa kwa Yesu
Kwetu ni uzima;
Mali, na tumai letu
Tunu ya neema.
Home