Na Pentekoste ya Kale

Na Pentekoste ya kale,
Watu walijazwa;
Moto wako ulishuka,
Leo twautaka.

Bwana, utujalie
Na nguvu zako tele,
Baraka za kale utufungulie;
Bwana utujalie
Na nguvu zako tele,
Waovu waokoke na
tuimbe shangwe.

Kazi na itayarishwe,
Kwako itendeke;
Bwana utuimarishe,
Na tusianguke.

Ziharibu dhambi zote,
Na utujalie;
Tufanye kazi na bidii,
Kwako kwa milele.

Useme nasi Ee, Bwana,
Tukikungojea;
Hatutakuacha hata
Tupewe baraka.

Home