Akifa Yesu Nikafa Naye
Akifa Yesu nikafa naye,
Uzima upya huishi naye;
Humtazama mpaka aje:
Nyakati zote ni wake Yeye.
Chorus
Nyakati zote nimo pendoni,
Nyakati zote ni uzimani,
Humtazama hata atokee,
Nyakati zote mimi ni wake.
Vita sipigi visivyo haki,
Na Bwana wangu hapiganiki;
Beramu yake haitwaliki,
Napo popote hila sitaki.
Sina mashaka, akawa mbali;
Mizigo yote aihimili;
Ananituliza Imanweli,
Nyakati zote mimi husali.
Sina huzuni na mimi sidhii:
Simwagi chozi, wala siguni:
Sikuti afa, ila kitini
Daima hunifikiri mimi.
Kila unyonge huusikia:
Kila ugonjwa kwake hupoa;
Yesu ni Mwenye kuniokoa
Nyakati zote hunijalia.
Home