Panda Asubuhi

Panda asubuhi mbegu ya fadhili,
Panda adhuhuri, tena jioni;
Tutaingojea siku ya mavuno,
Tutafurahi kuleta mavuno.

Chorus
Leta mavuno, leta mavuno,
Tutafurahi kuleta mavuno;
Leta mavuno, leta mavuno,
Tutafurahi kuleta mavuno.

Na panda mwangani, tena kivulini,
Usiwe na hofu kwa baridi mkuu;
Na mwisho wa kazi kuvuna mavuno,
Tutafurahi kuleta mavuno.

Mvunieni Bwana kwa machozi mengi,
Ijapo twaona taabu nyingi;
Mwisho wa kilio tutakaribishwa,
Tutafurahi kuleta mavuno.

Home





Next song