Nitaimba juu ya Mkombozi

Nitaimba juu ya Mkombozi,
Jinsi alivyonipenda;
Aliteswa msalabani,
Nisipate kulaaniwa.

Chorus
Imbeni juu ya Mkombozi,
Kwa damu aniweka;
Nafidiwa msalabani
Deni zangu zafutwa.

Nitanena habari njema,
Jinsi nilivyookoka;
Kwa upendo na neema,
Anipatia fidia.

Nltamsifu Mkombozi wangu,
Jinsi atoavyo ushindi:
Kwa uwezo namshangilia;
Juu ya dhambi na mauti.

Nitamsifu Mkombozi wangu
Jinsi alivyonipenda;
Amenitolea uzima,
Nikae kwake daima.

Home





Next song