Njoni na Furaha

Njoni na furaha, Enyi wa Imani,
Njoni Bethlehernu upesi!
Amezaliwa jumbe la Mbinguni
Njoni tumuabudu, Njoni tumuabudu,
Njoni tumuabudu Mwokozi.

Mungu wa waungu, Mwanga wa mianga,
Amekuwa radhi kuzaliwa;
Mungu wa kweli, wala si kiumbe
Njoni tumuabudu, Njoni tumuabudu,
Njoni tumuabudu Mwokozi.

Jeshi la mbinguni, Imbeni kwa nguvu!
Mbingu zote na zijae sifa!
Sifuni Mungu aliye mbinguni;
Njoni tumuabudu, Njoni tumuabudu,
Njoni tumuabudu Mwokozi.

Ewe Bwana Mwema, Twakubarikia,
Yesu, utukufu uwe wako;
Neno la Baba limekuwa mwili;
Njoni tumuabudu, Njoni turnuabudu
Njoni tumuabudu, Mwokozi.

Home





Next song