Nina Pumziko

Nina pumziko, maishani mwangu
Nafuraha tele ninayo,
Tangu niamue, kujisalimisha,
Kwa yesu yule wa ajabu

Ni wa maajabu, yehova yule mkuu
Hutukuzwa na malaika
Maselafi nao, wanamsujudu
Yesu yule wa maajabu

Msiwe na hofu, msiwe na shaka
Ninyi wana watakatifu
Maana tarubeta, itaitana
Ingieni rahani pangu

Upendo wangu, namutolea bwana
Ndiye chanzo cha imani yangu
Hunilisha vyema, malishoni bora
Kwa mito yenye maji hai

Sasa najitweka mikononi mwako
Ewe bwana uliyenifia,
Unipalilie na uniongoze, nifike uweponi mwako

Home