Kwake Yesu, Nakaa Salamani

Kwake Yesu, nakaa salamani,
Ijapokuwa giza na shida;
Nitamwamini, atanihifadhi,
Amenikomboa niwe wake.

Kwake Yesu, kwake Yesu,
Sitajitenga na Yeye;
Kwake Yesu, hapo nadumu,
Kwa salama ya milele.

Kwake Yesu, ninalo kimbilio,
Wakati nionapo huzuni;
Ataniponya nisifadhaike,
Nitakaa naye salamani.

Kwake Yesu iko furaha tele,
Nitaishi naye mpaka mwisho;
Atanilinda, sitashindwa kamwe,
Hunipa baraka na pumziko.

Home