Karibu Nawe, Ee Mwokozi

Karibu nawe, Ee Mwokozj,
Univute Bwana wa thamani;
lJnikaribishe moyoni,
Uniweke kwako salamani,
Uniweke kwako salamani.

Karibu nawe, sina kitu,
Sikuiletea sadaka kuu;
Nakujitolea kabisa,
Kwa damu nipate kutakaswa,
Kwa damu nipate kutakaswa.

Karibu nawe, Bwana wangu,
Niliuacha uovu'wangu;
Kiburi ehangu na anasa,
Namtaka Yesu aliye Bwana,
Namtaka Yesu aliye Bwana.

Karibu nawe, hata mwisho,
Nina salama ndani ya Kristo;
Mwokozi wangu kwa milele,
Nitakuwa karibu na wewe,
Nitakuwa karibu na wewe.

Home





Next song