Yesu Unipendaye
Yesu unipendaye
Kwako nakimbilia,
Ni Wewe utoshaye
Mwovu akinijia;
Yafiche ubavuni
Mwako maisha yangu;
Nifishe bandarini,
Wokoe moyo wangu.
Ngome nyingine sina;
Nategemea kwako.
Usinitupe Bwana,
Nipe neema yako,
Nsha kukwamania
Mwenye kuniwezesha;
Shari wanikingia,
Vitani wanitosha.
Nakutaka Mpaji
Vyote napata kwako;
Niwapo muhitaji,
Utanijaza vyako;
Nao waangukao
Wanyonge wape nguvu;
Poza wauguao,
Uongoze vipofu.
Bwana umeniosha
Moyo kwa damu yako;
Neema ya kutosha
Yapatikana kwako;
Kwako Bwana naona
Kisima cha uzima;
Mwangu moyoni, Bwana,
Bubujika daima.
Home