Anipenda Ni Kweli
Anipenda ni kweli:
Mungu anena hili;
Sisi wake watoto;
Kutulinda si zito.
Yesu anipenda,
Yesu anipenda,
Kweli anipenda
Mungu amesema.
Kwa kupenda akafa
Niokoke na kufa:
Atazisafi taka
Sana ataniweka.
Anipenda kabisa;
Niuguapo sasa
Anitunza rnbinguni
Niliyelala chini.
Kunipenda haachi
Tu sote hapa chini,
Baada ya mashaka
Kwake tanipeleka.
Home