Nyimbo na Tuziimbe Tena
Nyimbo na tuziimbe tena
Za alivyotupenda mbele;
Kwa damu ya thamani sana!
Mbinguni hwonana milele.
Chorus
Twonane milele,
Twonane bandarini kule;
Twonane milele,
Twonane bandarini kule.
Hupozwa kila aoshwaye
Kwa damu ya Kondoo yule;
Ataishi afurahiye
Vya Yesu mbinguni milele.
Hata sasa hufurahia
Tamu yake mapenzi yale,
Je, kwake tukifikiria,
Kutofarakana milele?
Twende mbele kwa Jina lake.
Hata aje Yesu ye yule,
Atatukaribisha kwake,
Tutawale naye milele.
Na beramu tuikunjue
Kumsifu Mwokozi yule,
Ili watu wote wajue
Wokovu u kwake milele.
Home