Mungu Mtukufu Aliye Bwana

Mungu Mtukufu aliye Bwana,
Akamtoa Yesu Mpendwa Mwana;
Akawa dhabihu kwa dhambi zote,
Kufungua njia kwa watu wote.

Chorus
Msifuni, msifuni,
Nchi imsikie;
Msifuni, msifuni,
Bwana mshangilie:
Njoni kwake Baba
Kwa Yesu Mwana,
Mpeni heshima
Aliye Bwana.

Ukombozi wetu, tendo Ia Mungu,
Ni ukamilifu kwa kila mtu;
Mwenye ukosefu akimwamini,
Atasamehewa na Yesu, kweli.

Ametufundisha mambo ya mbingu,
Tukafurahishwa na Mwana Mungu;
Ametuinua tukae naye,
Atatuongoza hata milele.

Home





Next song